KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMA E-mail: dvdmwk6@gmail..com SIMU: 0713 084 360

Wednesday, June 10, 2015

BENKI YA NBC YAZINDUA KAMPENI YA AKAUNTI ZA MISHAHARA.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Andrew Lyimo (katikati), akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya akaunti za mishahara iliyopewa jina la ‘Mcheza Kwao’ yenye lengo la kuhamasisha wafanyakazi kuchukulia misharahara benki. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja Huduma za Jamii wa benki hiyo, Irene Peter na Meneja Malipo ya Mishahara na Maendeleo, Amos Lyimo. 

 Meneja Malipo ya Mishahara na Maendeleo wa Benki ya NBC Tanzania, Amos Lyimo (kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya akaunti za mishahara iliyopewa jina la ‘Mcheza Kwao’ yenye lengo la kuhamasisha wafanyakazi kuchukulia misharahara benki. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi wa NBC, Andrew Lyimo na Meneja Huduma za Jamii wa benki hiyo, Irene Peter.

 Meneja Huduma za Jamii wa NBC, Irene Peter (kushoto), akizungumza wakati wa hafla hiyo. Kushoto kwake ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Wateja Binafsi, Andrew Lyimo na Meneja wa Malipo ya Mishahara na Maendeleo, Amos Lyimo.

 Baadhi ya waandishi waliohudhuria uzinduzi huo wakisikiliza maelezo kuhusu kampeni hiyo jijini Dar es Salaam leo.