KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMA E-mail: dvdmwk6@gmail..com SIMU: 0713 084 360

Friday, July 24, 2015

NBC YATOA ZAWADI KWA WASHINDI 35 WA DROO YA KWANZA YA KAMPENI YA MCHEZA KWAO.

 Meneja masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Alina Maria Kimaryo (wa pili kushoto) akizungumza wakati wa droo ya kwanza ya promosheni ya Kampeni ya akaunti za mishahara iliyopewa jina la ‘Mcheza Kwao’ jijini Dar es Salaam leo. Washindi 35 walijishindia zawadi mbalimbali za fedha taslimu na ofa za huduma ya mobile banking ya NBC. Kutoka kushoto ni Meneja katika Kitengo cha Bidhaa za Kuwekeza na Wateja Wakubwa, Dorothea Mabonye, Meneja Malipo ya Mishahara wa benki hiyo, Amos Lyimo na Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Humudi Abdulhussein.

 Meneja masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Alina Maria Kimaryo (kushoto) akipiga simu kwa mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya Kampeni ya akaunti za mishahara iliyopewa jina la ‘Mcheza Kwao’ jijini Dar es Salaam leo. Washindi 35 walijishindia zawadi mbalimbali za fedha taslimu na ofa za huduma ya mobile banking ya NBC. Kushoto kwake ni Meneja Malipo ya Mishahara wa benki hiyo, Amos Lyimo na Mkaguzi wa Bodi ya Michezio ya Kubahatisha, Humudi Abdulhussein.

 Meneja Malipo ya Mishahara wa Benki ya NBC, Amos Lyimo (katikati), akizungumza wakati wa droo ya kwanza ya promosheni ya Kampeni ya akaunti za mishahara iliyopewa jina la ‘Mcheza Kwao’ jijini Dar es Salaam leo. Washindi 35 walijishindia zawadi mbalimbali za fedha taslimu na ofa za huduma ya mobile banking ya NBC. Kushoto ni Meneja masoko wa benki hiyo, Alina Maria Kimaryo na Mkaguzi wa Bodi ya Michezio ya Kubahatisha, Humudi Abdulhussein.